Title : Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi
link : Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi
Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi
AC Milan ilipambana kutoka nyuma kwa mabao 2-0 na kuvuna pointi moja baada ya kuilazimisha Torino sare ya mabao 2-2 kisha kupanda hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa Serie A.
Bao la 14 la Andrea Belotti msimu huu na bao la Marco Benassi yaliipa Torino uongozi.
Mlinda mlango kinda wa Milan Gianluigi Donnarumma, 17, alifanya kazi ya ziada kuokoa mkwaju wa penalti ya Adem Ljajic kuwazuia wenyeji kuongoza kwa mabao 3-0.
Andrea Bertolacci akapunguza idadi ya mabao kwa wageni - ambao walimaliza mchezo wakiwa 10 - kabla ya mkwaju wa penalti ya Carlos Bacca kufanya matokeo kuwa mabao 2-2.
Milan, ambayo ilimpoteza Alessio Romagnoli dakika 89 kwa kadi mbili za manjano, inakaa juu ya mahasimu wao Inter kwa pointi moja na pointi nane nyuma ya vinara Juventus.
Torino, ambayo ilitupwa nje ya Coppa Italia na wapinzani hao wiki iliyopita, wako nyuma ya vinara kwa pointi 15.
Thus articles Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi
that is all articles Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi This time, hopefully can provide benefits to you all. Okay, see you in another article post.
You are now reading the article Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi the link address https://allnewsinformationtime.blogspot.com/2017/01/serie-torino-2-2-ac-milan-milan-yatoka.html
0 Response to "Serie A: Torino 2-2 AC Milan: Milan yatoka nyuma na kugawana pointi"
Post a Comment