Title : VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
link : VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo Februari 3, kwa mchezo mmoja ambapo mabingwa watetezi Young Africans watakuwa wenyeji wa Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ligi hiyo itaendelea Jumamosi Februari 4, kwa mechi mbili ambapo Wagonga Nyundo wa jiji la Mbeya, Mbeya City Council F.C wakiwakaribisha JKT Ruvu kwenye mchezo utakaopigwa uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Mchezo mwingine utapigwa kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea ambapo 'Wana Lizombe' Majimaji FC wakiwa wenyeji wa Simba SC.
Jumapili kutakuwa na mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Ndanda FC kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam – mchezo unaotarajiwa kuanza saa 1.00 usiku.
Aidha, Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja ambao utazikutanisha Toto Africans ya Mwanza dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Aidha, Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja ambao utazikutanisha Toto Africans ya Mwanza dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Thus articles VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
that is all articles VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara This time, hopefully can provide benefits to you all. Okay, see you in another article post.
You are now reading the article VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara the link address https://allnewsinformationtime.blogspot.com/2017/02/vpl-mechi-za-wikiendi-hii-ligi-kuu-ya.html
0 Response to "VPL: Mechi za wikiendi hii Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara"
Post a Comment